Showing posts with label menu kaisari yaliyo yake. Catholic song. Show all posts
Showing posts with label menu kaisari yaliyo yake. Catholic song. Show all posts

Thursday, 26 November 2015

Vipaji tumepewa

stanza one.
Vipaji  tumepewa, mapato  tumepata  lakini  binadamu  tunashindwa  kushukuru
Wakati  tunaomba  tunajinyonyekeza lakini  tumepata mikono  yetu  birika.

Chorus :
Mpeni  kaisari  yaliyo  yake ;mpeni Mungu  yaliyo  yake  Mungu *2

Stanza two.
Mifugo  tunafunga  nafaka  tunavuna  lakini  kila  siku tunakula  na kusazo;
Kumbuka  Kuna  wale  wasio  na chochote  hawawezi  kupata  hata  kikombe  cha  maji..

Stanza  three.
Tunapofanya  kazi  twapata  mishahara, shughuli  zetu  kwanza  kuingia  kwenye  baa;
Ikiwa  zitabaki, twakuja  kanisani  twamtolea  Mungu  shilingi  moja  na tano.

Stanza  four :
Tukiwa  na  wagonjwa  hatuwasaidii  Wakati  wamekufa  tunachanga  kwa huzuni ;
Twachukua  mikopo  kwa  mambo  ya  anasa, ujenzi  wa  kanisa  twalazimishwa  kutoa.
.
Stanza  five :
Kumbuka  Ibrahim  alimtoa  mwanao  kama  sadaka  tosha  kwake  Mungu  WA  mbinguni ;
Na sisi  kwa  furaha  tupeleke  sadaka  itayopendeza kama Ile  ya Abeli.